Mikopo kwa Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu
Submitted by Mwananchi on Mon, 2006-09-25 15:31.
Elimu
Jina
Respicius Didace
Maoni
Suala la mikopo kwa wanafunzi wa taasisi za Elimu ya Juu sasa hivi ni tatizo ambalo limetawala vyombo vya habari. Ni maoni yangu kuwa kabla ya kusema kuwa wanaofaa kupata mkopo ni wale wanafunzi wenye DIVISION ONE (Wanaume) au DIVISION ONE na DIVISION TWO (Wanawake)ni lazima tufuatilie huko vyuoni kuona kama hayo matokeo ya kidato cha sita yana uhalisia katika matokeo ya vyuoni. Hapa namaanisha kama ni kweli waliopata DIVISION ONE huendelea kuongoza )vyuoni. Mimi naamini kuwa kuna wanafunzi wanapata madaraja ya chini kulingana na aina ya shule wanazosomea au kwa sababu nyingine mbalimbali, hawa wanapokuja vyuoni pengine na DIVISION TWO au THREE zao hufanya vizuri sana hata kuliko wale wa DIVISION ONE. Kutoa mikopo kwa madaraja kutawakosesha watoto wa walalahoi haki yao yamsingi ya elimu. Nadhani pia, ni kuwahukumu bila kuwasikiliza. Naamini siku moja tutakuja kuulizwa tulisema nini kuhusu haya. Siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.
