Rushwa
RUSHWA ADUI WA HAKI MPAKA LINI?
Submitted by Mwananchi on Thu, 2007-01-25 13:02. RushwaJina
ALEXANDER HAULE
Maoni
RUSHWA:
Maoni yangu jamani tuipinge rushwa kwani ni adui wa haki.Utakuta familia inateseka kufuatilia mirathi mahakamani miaka 2 bila mafanikio,mara watakwambia faili lenu halionekani,mara ooh bado halijafika,yaaani hatuwaelewi hiki chombo kimeweka kwa madhumuni gani ?kutetea wanyonge au kuwakandamiza kabisa?
ALAFU SIONI KABISA KAZI WANAOIFANYA HAWA TAASISI YA KUZUIA RUSHWA(PCB),SIJUI WANAOGOPA AU HAWAWEZI MAJUKUMU YAO?
Simu
0713237512
rushwa
Submitted by Mwananchi on Mon, 2007-01-15 10:22. RushwaJina
juma richard okumu
Maoni
kwa kweli suala la rushwa limekuwa ni suala kubwa sana kwa sababu linagusa jamii nzima mfano kwenye vituo vya afya na vituo vya polisi kumekuwepo na vitendo vya rushwa kwa maana hiyo tunaomba serikali ihangalie suala hilo.hasa hapa kwetu musoma na sehemu mbalimbali tanzania.
Simu
RUSHWA
Submitted by Mwananchi on Mon, 2006-12-18 15:44. RushwaJina
JUMA RICHARD OKUMU
Maoni
NINAIOMBA SERIKALI IANGALIE SUALA LA RUSHWA HASA KATIKA VYOMBO VYA USALAMA WA RAIA KAMA MAHAKAMANI, POLISI NA MAMLAKA YA MAPATO KWA SABABU RUSHWA IMEKITHIRI SANA SEHEMU HIZO.
Simu
Rushwa CHUO KIKUU
Submitted by Mwananchi on Tue, 2006-10-31 11:39. RushwaJina
Eliya Wilbert
Maoni
Ninapenda kutoa maoni/malalamiko yangu kuhusu RUSHWA ya kupata vyumba inayoendelea pale CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM. Kwa kweli ni AIBU kwa wanavyuo KUUZIWA vyumba kwa bei inayoanzia 200,000/ hadi 500,000/ kwa njia isiyo halali. Ninasema hivyo kwa sababu jambo hili limetokea katika semister hii inayoendelea sasa, ma-warden wa mabweni wanadiriki KUWAUZIA wanafunzi vyumba hivyo ambavyo ni HAKI YAO kuvipata kwa taratibu zilizowekwa na utawala wa chuo. Tena kuna kila dalili za UCHAFU huu kuendelea katika semister ijayo. Ninawashauri HAKI ELIMU kufuatilia ninyi wenyewe tena hata kwa kuwahoji baadhi ya wanafunzi hasa wanaoishi HALL VII. Kama wanafunzi hawa watakuwa viongozi hapo baadae, tutegemee RUSHWA kutokuisha Tanzania. Kwani pale walipo wanachukua kozi ya KUTOA NA KUPOKEA rushwa, na hasa ukizingatia kuwa hakuna anayejali wala kufuatilia suala hili. Tunawaomba sana mfuatilie jambo hili na kulifikisha kwenye vyombo vya habari ili kuliokoa taifa letu na mdudu huyu hatari aitwaye RUSHWA.
Simu
Rushwa
Submitted by Mwananchi on Sun, 2006-08-27 16:00. RushwaJina
GREYSON ONESMO
Maoni
Mimi ni kijana wa umri wa miaka 16 ninasoma Kampala. Huwa ninarudi kila likizo.Nimeshuhudia mambo mengi yasiyo na utu katikan mipaka ya Tanzania na Kenya. Kusema ukweli inatia huruma na tunaomba serekali iingilie kati.
Simu
Lilian, Dar es Salaam
RushwaSwala la rushwa limekithiri hapa nchini. Unaenda kutafuta kazi, una vyeti vyako vizuri, umesoma. Unavyoenda kule maofisini, unaenda unanza kuambiwa: unipe kiasi fulani cha pesa, ambacho hicho inakuwa ni kama inaathari wananchi. Na watu, inakuwa mambo mengine ya ufuatiliaji ambao hauna maana. Kumbe, matokeo yake unakuta wale watu wana ndugu zao ambao hawana hata kazi, wanachukua vyeti wanavifoji.
We have a big corruption issue in this country. You go to look for a job, you have good certificates, are well-educated. When you come to the office, they start by saying: give me a certain amount of money, which is affecting the citizens in a negative way. And these people will come up with other things to follow up for no reason. Surprise, in the end you find out that these people have relatives without qualifications...
