Daladala
Abdalla, Mbeya
DaladalaKwa sababu ni mfanyakazi eneo la Stend, kero langu lipo kwa gari zinatoka Tunduma, zinatoka Kiera, zinatoka Chunya zinaishia Mwanjila wakati kuna Stend kuu hapa yakufika watu kuja kupokea ndugu zao, hasa hapa watu wanapata tabu kuja kuwatafuta ndugu zao. Ndugu yako ametoka wapi, ametoka Kiela inabidi apate tabu tena kutoka hapa aende tena Mwanjila kwenda kumtafuta ndugu yake wakati hapa kuna Stend kuu ipo hapa Mbeya.
As I work at the bus stop, I am irritated about the public transport vehicles from Tunduma, Kiero and Chunya that terminates the journey at Mwanjila, whereas there is a main bus terminal here in Mbeya where relatives and friends wait to receive the passengers.
Mohamed, Iringa
DaladalaKubwa linalonikera, ni kwamba hao madereva wa Haisi wanachukua gari asubuhi ikifika majira ya saa kumi au saa kumi na moja jioni wanaondoka na kuwaachia watu ambao hawana leseni maarufu kwa jina la dai waka...
What infuriates me most, is that our public transport drivers take the minibuses from morning to four or five o'clock in the afternoon, then they leave their vehicles to untrained drivers without licences, widely know as day workers...
Daladala
Submitted by Mwananchi on Wed, 2006-10-18 15:32. DaladalaJina
Tupa jb
Maoni
Unajua hapa Tanga hakuna bei maalum ya daladala mara 200 mara 300 wakati tunajua Dar nauli inaanzia 150 mpaka 250 kutokana na umbali kwanza walisema watashusha bei kwa kuwa mafuta bado yapo kwenye visima wamenunua kwa bei kubwa pamoja na kodi kubwa sasa sijui mpaka sasa mafuta hayajaisha kwenye visima hivyo ningeomba mamlaka husika ifuatilie tujue bei ni kiasi gani si mpaka uombe ndio ulipe 200
Simu
Leseni kwa madereva kuepusha ajali
Submitted by Mwananchi on Fri, 2006-10-06 21:25. DaladalaJina
Sosteness Emanuely Kawishe
Maoni
Mimi naonelea kwamba dereva yoyote anaendesha gari ya abiria na mizigo zaidi tani mbili awe na leseni ya class c na awe umri usiopungua miaka thelathini na tano na awe amesoma chuo kinachoeleweka kiserikali na kiundwe chombo maalum cha kuhakiki leseni.
Simu
0713439692
biashara ya daladala
Submitted by Mwananchi on Wed, 2006-09-06 09:42. Biashara | DaladalaJina
mack
Maoni
wafanyabiashara wa daladala mkoani moshi wamekuwa wakiendelea kulipisha nauli ile ile ambayo ilichangiwa na mafuta kupanda bei licha ya serikali kupunguza gharama zote zilizo changia upandishwajiwa nauli hiyo.Ninaomba vyombo husika viliangalie hili na ikiwezekana watoe ufafanuzi wa kutosha kuhusiana na swala hili la kutoshusha naulikwani bado ni kikwazo kwa sisi ambao mapato yetu yapo chini.
Simu
Makonda wa daladala
Submitted by Mwananchi on Mon, 2006-09-04 13:53. Afya | DaladalaJina
sudi jongo
Maoni
maoni yangu ni kwa makonda wa daladala na mabasi ya usafiri kwa ujumla hapa nchini, Nilikuwa naomba serikali iwapatie adhabu makonda na madereva ambao hawavai uniform na wanaovaa ovyo uniform zao, pia aslimia 87 ya makonda daladala hawafui uniform zao mpaka kupelea harufu mbaya mtu uingiapo ndani ya gari kwa ajili ya kusafili. Wakumbuke kwamba ile ni kazi yao na wanapaswa kuithamini, kwani wengi wao wanaangaika hawana ajira, sasa wao kwanini wasifanye kazi kwa moyo wa usafi ikiwa ni sehemu pia ambayo inaleta changamoto katika maendeleo ya taifa letu?
Simu
0744 522 640
